Recent Comments

NEWS:MUHIDINI GURUMO AMETANGAZA RASMI KUSTAAFU MUZIKI

MWANA MUZIKI mkongwe wa bendi ya muziki ya Msondo Ngoma Maalim Muhidini
Gurumo  ametangaza rasmi kuachana  na kazi ya muziki  baada ya kutoa albamu ya 60 tangu aanze kuimba nyimbo hapa nchini.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari  jijijini Dar es Salaam hapo jana, Gurumo amesema kuwa  kutokana  na kuifanya  kazi ya muziki kwa miaka 53, ameamua kustaafu na  kuwaachia vijana waendelee na kazi hiyo.
Amesema kuwa kwa muda mrefu alikuwa nje ya familia yake kutokana na kurudi usiku wa  manane  hivyo kitendo cha kustaafu muziki  kitamsaidia  kwa asilimia kubwa  kuwa  karibu na familia  yake

Share on Google Plus

About Wasafi

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment